Zaburi 53

Zaburi 53

Zaburi 53

Uovu wa wanadamu

(Za 14)

1Mpumbavu anasema moyoni mwake,

“Hakuna Mungu.”

Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa,

hakuna hata mmoja atendaye mema.

2Mungu anawachungulia wanadamu chini

kutoka mbinguni

aone kama wako wenye akili,

wowote wanaomtafuta Mungu.

3Kila mmoja amegeukia mbali,

wameharibika wote pamoja,

hakuna atendaye mema.

Naam, hakuna hata mmoja!

4Je, watendao maovu kamwe hawatajifunza:

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

hao ambao hawamwiti Mungu?

5Hapo waliingiwa na hofu kuu,

ambapo hapakuwa na hofu.

Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia;

uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.

6Laiti wokovu wa Israeli ungekuja kutoka Sayuni!

Mungu anaporejesha wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.