Zaburi 93

Zaburi 93

Zaburi 93

Mungu ni mkuu

1Bwana anatawala, amejivika utukufu;

Bwana amejivika utukufu

tena amejivika nguvu.

Dunia imewekwa imara,

haitaondoshwa.

2Kiti chako cha enzi kimekuwa thabiti tangu zamani;

wewe umekuwa tangu milele.

3Bahari zimepaza, Ee Bwana ,

bahari zimepaza sauti zake;

bahari zimepaza sauti za mawimbi yake.

4Yeye ni mkuu kuliko ngurumo ya maji makuu,

ni mkuu kuliko mawimbi ya bahari:

Bwana aishiye juu sana ni mkuu.

5Ee Bwana , sheria zako ni imara;

utakatifu umepamba nyumba yako

pasipo mwisho.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.