Zaburi 98

Zaburi 98

Zaburi 98

Mungu Mtawala wa dunia

1Mwimbieni Bwana wimbo mpya,

kwa maana ametenda mambo ya ajabu;

kitanga chake cha kuume na mkono wake mtakatifu

umemfanyia wokovu.

2Bwana ameufanya wokovu wake ujulikane

na amedhihirisha haki yake kwa mataifa.

3Ameukumbuka upendo wake

na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli;

miisho yote ya dunia imeuona

wokovu wa Mungu wetu.

4Mpigieni Bwana kelele za shangwe, dunia yote,

ipaze sauti kwa nyimbo za shangwe na vinanda;

5mwimbieni Bwana kwa kinubi,

kwa kinubi na sauti za kuimba,

6kwa tarumbeta na mvumo wa baragumu za pembe za kondoo dume:

shangilieni kwa furaha mbele za Bwana , aliye Mfalme.

7Bahari na ivume na kila kilicho ndani yake,

dunia na wote wanaoishi ndani yake.

8Mito na ipige makofi,

milima na iimbe pamoja kwa furaha,

9vyote na viimbe mbele za Bwana ,

kwa maana yuaja kuhukumu dunia.

Atahukumu dunia kwa haki

na mataifa kwa haki.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.