The chat will start when you send the first message.
1Nimekuinulia macho yangu,
Wewe uketiye mbinguni.
2Kama vile macho ya watumishi
Yanavyoutegemea mkono wa bwana zao
Kama macho ya mjakazi
Yanavyoutegemea mkono wa bibi yake;
Ndivyo macho yetu yanavyomtegemea BWANA, Mungu wetu,
Hadi atakapoturehemu.
3Uturehemu, Ee BWANA, uturehemu sisi,
Kwa maana tumeshiba dharau.
4Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha,
Na dharau ya wenye kiburi.