Zaburi 131

Zaburi 131

Kumtumainia Mungu kwa utulivu

1BWANA, moyo wangu hauna kiburi,[#Rum 12:16]

Wala macho yangu hayainuki.

Wala sijishughulishi na mambo makuu,

Wala mambo yanayozidi nguvu zangu.

2Hakika nimeituliza nafsi yangu,[#Mt 18:3]

Na kuinyamazisha.

Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya

Kifuani mwa mama yake;

Roho yangu ni kama mtoto,

Aliyeachishwa kunyonya.

3Ee Israeli, umtarajie BWANA,

Tangu leo na hata milele.

The Holy Bible in Kiswahili, Revised Union Version © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 2013. 
Published by: Bible Society of Tanzania