Tobiti 9

Tobiti 9

NDOA YA TOBIA

Fedha zarudishwa

1Kwa hiyo Tobia akamwita Rafaeli, akamwambia,

2Ndugu yangu Azaria, utwae mtumishi mmoja na ngamia wawili, uende Rage, mji wa Umedi,

3kwa Gabaeli, ili uniletee ile fedha; tena uje naye kwenye karamu ya harusi. Yaani, Ragueli ameapa nisiondoke mimi.

4Ati! Baba yangu anazihesabu siku, nami nikikawia sana atahuzunika mno.

5Hivyo Rafaeli akaondoka, akaenda akatua kwa Gabaeli, akampa ile hati. Naye akaileta ile mifuko ya fedha yenye mihuri yake, akampa.

6Asubuhi mapema wakaondoka wote wawili wakafika kwenye karamu ya harusi; naye Gabaeli akambariki Tobia na mkewe.

The Holy Bible in Kiswahili, Revised Union Version © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 2013. 
Published by: Bible Society of Tanzania