The chat will start when you send the first message.
1Mpaka lini, Bwana, utanisahau kila mara? Mpaka lini utauficha uso wako, usinione?[#Sh. 77:8; Hab. 1:2.]
2Mpaka lini nitie wasiwasi rohoni mwangu na masikitiko moyoni mwangu kila siku? Mpaka lini ataniinukia mchukivu wangu?
3Nitazame, ukaniitikie, Bwana Mungu wangu! Yaangaze macho yangu, nisipatwe na usingizi uuao!
4Mchukivu wangu asiseme: Nimemshinda! Nao wanisongao wasishangilie, ya kuwa nimetikisika!
5Nami nimeuegemea upole wako; moyo wangu hushangilia, ya kuwa unaniokoa; nitamwimbia Bwana kwa ajili ya mema, aliyonitendea.[#Sh. 9:15.]