Yona 2

Yona 2

Wimbo wa kushukuru

1Ndipo Yona akamwomba BWANA, Mungu wake, akiwa katika tumbo la yule samaki,

2Akasema,

Nilimlilia BWANA kwa sababu ya shida yangu,

Naye akaniitikia;

Katika tumbo la kuzimu niliomba,

Nawe ukasikia sauti yangu.

3Maana ulinitupa vilindini,[#Zab 88:6]

Ndani ya moyo wa bahari;

Gharika ya maji ikanizunguka pande zote;

Mawimbi yako yote na gharika zako zote zimepita juu yangu.

4Nami nikasema, Nimetupwa mbali na macho yako;[#Zab 31:22; Isa 49:14; 1 Fal 8:38]

Lakini nitatazama tena kukabili hekalu lako takatifu.

5Maji yalinizunguka, hata nafsini mwangu;

Vilindi vilinizunguka;

Mwani ulikizinga kichwa changu;

6Nilishuka hata pande za chini za milima;

Hiyo nchi ambayo mapingo yake yanafunga hata milele;

Lakini umeipandisha nafsi yangu kutoka humo shimoni,

Ee BWANA, Mungu wangu,

7Roho yangu ilipozimia ndani yangu,[#Zab 18:6; 34:6; 130:2; Yer 2:13]

Nilimkumbuka BWANA;

Maombi yangu yakakufikia,

Katika hekalu lako takatifu.

8Watu waangaliao mambo ya ubatili na uongo[#2 Fal 17:15; Zab 31:6; Yer 10:8]

Hujitenga na rehema zao wenyewe.

9Lakini mimi nitakutolea sadaka kwa sauti ya shukrani;[#Zab 50:14; 66:13-15; Hos 14:2; Ebr 13:15]

Nitaziondoa nadhiri zangu.

Wokovu hutoka kwa BWANA.

10BWANA akasema na yule samaki, naye akamtapika Yona katika pwani.[#Yon 1:17; Mt 8:9]

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya