Zaburi 100

Zaburi 100

Nchi zote zaitwa kumsifu Mungu

1Mshangilieni BWANA, enyi nchi zote;

2Mtumikieni BWANA kwa furaha;

Njoni mbele zake mkiimba;

3Jueni kwamba BWANA ndiye Mungu;[#Ayu 10:8,9; Mhu 12:1; Efe 2:10; Eze 34:30]

Ndiye aliyetuumba na sisi tu watu wake;

Tu watu wake, na kondoo wa malisho yake.

4Ingieni malangoni mwake kwa shukrani;

Nyuani mwake kwa kusifu;

Mshukuruni, lihimidini jina lake;

5Maana BWANA ni mwema;[#1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 106:1; 107:1; 118:1; 136:1; Yer 33:11]

Rehema zake ni za milele;

Na uaminifu wake katika vizazi vyote.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya