Zaburi 128

Zaburi 128

Nyumba ya mwumini yenye furaha

1Heri kila mtu amchaye BWANA,

Aendaye katika njia yake.

2Taabu ya mikono yako hakika utaila;[#Isa 3:10]

Utakuwa heri, na kwako kwema.

3Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,

Katika nyumba yako.

Wanao watakuwa kama miche ya mizeituni

Wakiizunguka meza yako.

4Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA.

5BWANA akubariki toka Sayuni;[#Zab 134:3]

Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;

6Naam, ukawaone wana wa wanao.[#Mwa 50:23]

Amani ikae na Israeli.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya