The chat will start when you send the first message.
1Ee BWANA, toka vilindini nimekulilia.[#Omb 3:55; Yon 2:2]
2Bwana, uisikie sauti yangu.
Masikio yako na yaisikilize
Sauti ya dua zangu.
3BWANA, kama Wewe ungehesabu maovu,[#Zab 143:2; Yn 8:7-9; Rum 3:20]
Ee Bwana, nani angesimama?
4Lakini kwako kuna msamaha,[#2 The 1:6; Zab 37:2; Yer 17:6; Kut 3:4-7; Efe 1:7; 1 Fal 8:40; Yer 33:8,9; Ebr 12:28]
Ili Wewe uogopwe.
5Nimemngoja BWANA, roho yangu imengoja,[#Isa 26:8]
Na neno lake nimelitumainia.
6Nafsi yangu inamngoja Bwana,
Kuliko walinzi waingojavyo asubuhi,
Naam, walinzi waingojao asubuhi.
7Ee Israeli, umtarajie BWANA;[#Isa 55:7]
Maana kwa BWANA kuna fadhili,
Na kwake kuna ukombozi mwingi.
8Yeye atamkomboa Israeli na maovu yake yote.[#Mt 1:21; Tit 2:14]