Zaburi 136

Zaburi 136

Uumbaji wa Mungu na matukio ya kihistoria

1Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema;[#1 Nya 16:34; 2 Nya 5:13; 7:3; Ezr 3:11; Zab 100:5; 106:1; 107:1; 118:1; Yer 33:11]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

2Mshukuruni Mungu wa miungu;[#Kut 18:11; Kum 10:17]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

3Mshukuruni Bwana wa mabwana;[#1 Tim 6:15; Ufu 17:14]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

4Yeye peke yake afanya maajabu makuu;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

5Yeye aliyeumba mbingu kwa fahamu zake;[#Mwa 1:1; Mit 3:19]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

6Yeye aliyeitandaza nchi juu ya maji;[#Mwa 1:2; Yer 10:12]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

7Yeye aliyeumba mianga mikubwa;[#Mwa 1:16; Kum 4:19]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

8Jua litawale mchana;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

9Mwezi na nyota zitawale usiku;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

10Yeye aliyewapiga Wamisri kwa kuwaua wazaliwa wao wa kwanza;[#Kut 12:29]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

11Akawatoa Waisraeli katikati yao;[#Kut 12:51]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

12Kwa mkono hodari na mkono ulionyoshwa;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

13Yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu;[#Zab 78:13; Kut 14:21-29]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

14Akawavusha Israeli katikati yake;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

15Akamwangusha Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

16Yeye aliyewaongoza watu wake jangwani;[#Kum 8:15]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

17Yeye aliyewapiga wafalme wakuu;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

18Akawaua wafalme mashuhuri;[#Kum 29:7]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

19Sihoni, mfalme wa Waamori;[#Hes 21:21-30]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

20Na Ogu, mfalme wa Bashani;[#Hes 21:31-35]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

21Akaitoa nchi yao iwe urithi;[#Yos 12:1]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

22Urithi wa Israeli mtumishi wake;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

23Aliyetukumbuka katika unyonge wetu;[#Mwa 8:1; Kum 32:36; Zab 102:17; Isa 63:9; Lk 1:48]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

24Akatuokoa na watesi wetu;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

25Yeye akipaye kila kiumbe chakula chake;[#Zab 104:27]

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

26Mshukuruni Mungu wa mbingu;

Kwa maana fadhili zake ni za milele.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya