Zaburi 47

Zaburi 47

Utawala wa Mungu juu ya mataifa

1Enyi watu wote, pigeni makofi,

Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.

2Kwa kuwa BWANA Aliye Juu, mwenye kuogofya,[#Kum 7:21; Neh 1:5; Mal 1:14]

Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.

3Amewatiisha watu wa nchi chini yetu,[#Zab 18:47]

Na mataifa chini ya miguu yetu.

4Ametuchagulia urithi wetu,[#1 Pet 1:4]

Fahari ya Yakobo ampendaye.

5Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,[#Zab 24:7-10; Mdo 1:9; Efe 4:8-10; 1 Tim 3:16]

BWANA kwa sauti ya baragumu.

6Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa;

Imbeni sifa kwa mfalme wetu, imbeni sifa.

7Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,[#Zek 14:9; 1 Kor 14:15]

Imbeni kwa zaburi.

8Mungu ayatawala mataifa,

Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.

9Wakuu wa watu wamekusanyika,

Kama watu wa Mungu wa Abrahamu.

Maana ngao za dunia zina Mungu,

Ametukuka sana.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya