Zaburi 56

Zaburi 56

Kumtumaini Mungu katika mateso

1Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza,[#Zab 31:9]

Mchana kutwa ananionea akileta vita.

2Adui zangu wanataka kunimeza mchana kutwa,[#Zab 57:3]

Maana ni wengi wanaonipiga vita.

3Siku ya hofu yangu nitakutumaini Wewe;[#1 Sam 30:6; 2 Nya 20:3]

4Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake.[#Ebr 13:5,6]

Nimemtumaini Mungu, sitaogopa;

Mwenye mwili atanitenda nini?

5Mchana kutwa wanapotosha maneno yangu,

Mawazo yao yote ni juu yangu kunitakia mabaya.

6Hukutanika, hujificha, huziangalia nyayo zangu,[#Mdo 4:27,28]

Kwa kuwa waliniotea ili waniue.

7Je! Wataokoka kwa uovu wao?

Ee Mungu, uwaangamize kwa hasira yako.

8Umehesabu kutangatanga kwangu;[#Mal 3:16]

Uyatie machozi yangu katika chupa yako;

(Je! Hayamo katika kitabu chako?)

9Ndipo adui zangu watarudi nyuma siku ile niitapo.[#Isa 8:9,10]

Neno hili najua kuwa MUNGU yu upande wangu;

10Kwa msaada wa MUNGU nitalisifu neno lake.

Kwa msaada wa BWANA nitalisifu neno lake.

11Nimemtumaini Mungu, sitaogopa;

Mwanadamu atanitenda nini?

12Ee Mungu, nadhiri zako ziko juu yangu;[#Zab 116:14-16]

Nitakutolea dhabihu za kushukuru.

13Maana umeniponya nafsi yangu na mauti;[#Ayu 33:30]

Je! Hukuizuia miguu yangu isianguke?

Ili niende mbele za Mungu

Katika nuru ya walio hai.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya