Zaburi 67

Zaburi 67

Mataifa yaitwa kumsifu Mungu

1Mungu na atufadhili na kutubariki,[#Zab 4:6; 31:16; 119:135; Hes 6:25,26; 2 Kor 4:6]

Na kutuangazia uso wake.

2Njia yake ijulikane duniani,[#Mdo 13:10; Tit 2:11; Lk 2:30-32]

Wokovu wake katikati ya mataifa yote.

3Watu na wakushukuru, Ee Mungu,[#Isa 24:15,16]

Watu wote na wakushukuru.

4Mataifa na washangilie,[#Zab 96:10]

Naam, waimbe kwa furaha,

Maana kwa haki utawahukumu watu,

Na kuwaongoza mataifa walioko duniani.

5Watu na wakushukuru, Ee Mungu,

Watu wote na wakushukuru.

6Nchi imetoa mazao yake[#Law 26:4; Isa 1:19; Zab 85:9-12]

MUNGU, Mungu wetu, ametubariki.

7Mungu atatubariki sisi;[#Zab 22:27]

Miisho yote ya dunia itamcha Yeye.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya