Zaburi 70

Zaburi 70

Sala ya ukombozi kutoka kwa adui

1Ee Mungu, uniokoe,

Ee BWANA, unisaidie hima.

2Waaibike, wafedheheke,[#Zab 109:29]

Wanaoitafuta nafsi yangu.

Warudishwe nyuma, watahayarishwe,

Wapendezwao na shari yangu.

3Warudi nyuma, na iwe aibu yao,

Wanaosema, Ewe! Ewe!

4Washangilie, wakufurahie,[#Isa 61:10; Hab 3:17; Rum 5:2; Flp 3:1; 1 Pet 1:2-9]

Wote wakutafutao.

Waupendao wokovu wako

Waseme daima, Atukuzwe Mungu.

5Nami ni maskini na mhitaji,[#Zab 40:17; Amu 5:28; Zab 141:1; Ebr 10:37; Ufu 22:20]

Ee Mungu, unijilie kwa haraka.

Ndiwe msaada wangu na mwokozi wangu,

Ee BWANA, usikawie.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya