Ayubu 25

Ayubu 25

Bildadi anasema: Mwanadamu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?

1Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu:

2“Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu;

yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.

3Je, majeshi yake yaweza kuhesabika?

Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?

4Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?

Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?

5Ikiwa hata mwezi sio mwangavu

nazo nyota si safi machoni pake,

6sembuse mtu ambaye ni funza:

mwanadamu ambaye ni buu tu!”

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.