The chat will start when you send the first message.
1Ndipo Bildadi Mshuhi akajibu:
2“Mamlaka na kuheshimiwa ni vyake Mungu;
yeye huthibitisha amani katika mbingu juu.
3Je, majeshi yake yaweza kuhesabika?
Ni nani asiyeangaziwa na nuru yake?
4Mtu awezaje kuwa mwadilifu mbele za Mungu?
Awezaje mtu aliyezaliwa na mwanamke kuwa safi?
5Ikiwa hata mwezi sio mwangavu
nazo nyota si safi machoni pake,
6sembuse mtu ambaye ni funza:
mwanadamu ambaye ni buu tu!”