Zaburi 123

Zaburi 123

Zaburi 123

Kuomba rehema

1Ninayainua macho yangu kwako,

kwako wewe unayeketi mbinguni kwenye kiti chako cha enzi.

2Kama vile macho ya watumwa

yatazamavyo mkono wa bwana wao,

kama vile macho ya mjakazi

yatazamavyo mkono wa bibi yake,

ndivyo macho yetu yamtazamavyo Mwenyezi Mungu, Mungu wetu,

hadi atakapotuhurumia.

3Uturehemu, Ee Mwenyezi Mungu, uturehemu,

kwa maana tumevumilia dharau nyingi.

4Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi,

dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.