Zaburi 131

Zaburi 131

Zaburi 131

Kumtegemea Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu

1Moyo wangu hauna kiburi, Ee Mwenyezi Mungu,

macho yangu hayajivuni;

sijishughulishi na mambo makuu kunizidi

wala mambo ya ajabu mno kwangu.

2Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya

ndivyo ilivyo nafsi iliyo ndani yangu.

3Ee Israeli, mtumaini Mwenyezi Mungu

tangu sasa na hata milele.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.