The chat will start when you send the first message.
1Ee Mungu, sikia kilio changu,
usikilize maombi yangu.
2Kutoka miisho ya dunia ninakuita,
ninakuita huku moyo wangu unadhoofika;
uniongoze kwenye mwamba
ulio juu kuniliko.
3Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu,
ngome imara dhidi ya adui.
4Natamani kukaa kwenye hema lako milele,
na kukimbilia chini ya uvuli wa mabawa yako.
5Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu,
umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.
6Mwongezee mfalme siku za maisha yake,
miaka yake kwa vizazi vingi.
7Mtawaze mbele za Mungu milele;
amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.
8Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako
na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.