Zaburi 61

Zaburi 61

Zaburi 61

Kuomba ulinzi

1Ee Mungu, sikia kilio changu,

usikilize maombi yangu.

2Kutoka miisho ya dunia ninakuita,

ninakuita huku moyo wangu unadhoofika;

uniongoze kwenye mwamba

ulio juu kuniliko.

3Kwa kuwa umekuwa kimbilio langu,

ngome imara dhidi ya adui.

4Natamani kukaa kwenye hema lako milele,

na kukimbilia chini ya uvuli wa mabawa yako.

5Ee Mungu, kwa kuwa umesikia nadhiri zangu,

umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.

6Mwongezee mfalme siku za maisha yake,

miaka yake kwa vizazi vingi.

7Mtawaze mbele za Mungu milele;

amuru upendo wako na uaminifu wako vimlinde.

8Ndipo daima nitaliimbia sifa jina lako

na kuzitimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.