Zaburi 75

Zaburi 75

Zaburi 75

Mungu ni mwamuzi

1Ee Mungu, tunakushukuru,

tunakushukuru wewe,

kwa kuwa jina lako li karibu;

watu husimulia matendo yako ya ajabu.

2Unasema, “Ninachagua wakati maalum;

ni mimi nihukumuye kwa haki.

3Dunia inapotetemeka na watu wake wote,

ni mimi ninayezishikilia nguzo zake imara.

4Kwa wale wenye majivuno ninasema,

‘Msijisifu tena,’

kwa wale waovu, ‘Msiinue pembe zenu.

5Msiinue pembe zenu dhidi ya mbingu;

msiseme kwa kiburi.’ ”

6Hakuna yeyote atokaye mashariki wala magharibi

au kutoka jangwani awezaye kumkweza mwanadamu.

7Bali Mungu ndiye ahukumuye:

Humshusha huyu na kumkweza mwingine.

8Mkononi mwa Bwana kuna kikombe

kilichojaa mvinyo unaotoka povu

uliochanganywa na vikolezo;

huumimina, nao waovu wote wa dunia

hunywa hata tone la mwisho.

9Bali mimi, nitatangaza hili milele;

nitaimba sifa kwa Mungu wa Yakobo.

10Nitazikatilia mbali pembe za waovu wote,

bali pembe za wenye haki zitainuliwa juu.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.