Zaburi 95

Zaburi 95

Zaburi 95

Wimbo wa kumsifu Mungu

1Njooni, tumwimbie Bwana kwa furaha;

tumfanyie kelele za shangwe

Mwamba wa wokovu wetu.

2Tuje mbele zake kwa shukrani,

tumtukuze kwa vinanda na nyimbo.

3Kwa kuwa Bwana ni Mungu mkuu,

mfalme mkuu juu ya miungu yote.

4Mkononi mwake mna vilindi vya dunia,

na vilele vya milima ni mali yake.

5Bahari ni yake, kwani ndiye aliyeifanya,

na mikono yake iliumba nchi kavu.

6Njooni, tusujudu, tumwabudu,

tupige magoti mbele za Bwana Muumba wetu,

7kwa maana yeye ndiye Mungu wetu,

na sisi ni watu wa malisho yake,

kondoo chini ya utunzaji wake.

Mkiisikia sauti yake leo,

8msiifanye mioyo yenu migumu

kama mlivyofanya kule Meriba,

kama mlivyofanya siku ile

kule Masa jangwani,

9ambapo baba zenu walinijaribu na kunipima,

ingawa walikuwa wameyaona matendo yangu.

10Kwa miaka arobaini nilikasirikia kizazi kile,

nikasema, “Hawa ni taifa ambalo mioyo yao imepotoka,

nao hawajazijua njia zangu.”

11Hivyo nikatangaza kwa kiapo katika hasira yangu,

“Kamwe hawataingia rahani mwangu.”

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.