Zaburi 93

Zaburi 93

Ukuu wa enzi ya Mungu

1BWANA ametamalaki, amejivika adhama,[#Isa 52:7; Ufu 19:6; Ayu 40:10; Zab 104:1; Isa 59:17]

BWANA amejivika, ukuu na nguvu, kama mavazi ya kifalme.

Naam, ulimwengu umethibitika usitikisike;

2Kiti chako kimekuwa thabiti tokea zamani;[#Mit 8:22]

Wewe ndiwe uliye tangu milele.

3Ee BWANA, mito imepaza,

Mito imepaza sauti zake,

Mito imepaza uvumi wake.

4Kupita sauti ya maji mengi, maji makuu,[#Zab 29:10]

Kupita mawimbi ya bahari yaumkayo,

BWANA Aliye Juu ndiye mwenye ukuu.

5Shuhuda zako ni amini sana;

Utakatifu ndio uifaao nyumba yako,

Ee BWANA, milele na milele.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya