Zaburi 61

Zaburi 61

Kuomba ulinzi

1Ee Mungu, usikie kilio changu,

usikilize sala yangu.

2Ninakulilia kutoka miisho ya dunia,

nikiwa nimevunjika moyo.

Uniongoze juu kwenye mwamba mkubwa

3maana wewe ndiwe kimbilio langu,

kinga yangu imara dhidi ya adui.

4Naomba nikae nyumbani mwako milele

nipate usalama chini ya mabawa yako.

5Ee Mungu, umezisikia ahadi zangu,

umenijalia sehemu yangu unayowapa wale wakuchao.

6Umjalie mfalme maisha marefu,

miaka yake iwe ya vizazi vingi.

7Atawale milele mbele yako, ee Mungu;

fadhili na uaminifu wako vimlinde.

8Hivyo nitakuimbia nyimbo za sifa,

nikizitekeleza ahadi zangu kila siku.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania