Zaburi 122

Zaburi 122

Sifa za Yerusalemu

1Nilifurahi waliponiambia:

“Twende nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.”

2Sasa tuko tumesimama,

kwenye malango yako, ee Yerusalemu!

3Yerusalemu, mji uliojengwa,

ili jumuiya ikutane humo.

4Humo ndimo makabila yanamofika,

naam, makabila ya Israeli,

kumshukuru Mwenyezi-Mungu kama alivyoagiza.

5Humo mmewekwa mahakama ya hukumu ya haki,

mahakama ya ukoo wa kifalme wa Daudi.

6Uombeeni Yerusalemu amani:

“Wote wakupendao na wafanikiwe!

7Ndani ya kuta zako kuwe na amani,

majumbani mwako kuweko usalama!”

8Kwa ajili ya jamaa na ndugu zangu,[#122:8 Hawa ni Waisraeli wenzi wa huyo Mwanazaburi ambao waliishi huko Yerusalemu.]

ee Yerusalemu, nakutakia amani!

9Kwa ajili ya nyumba ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,

ninakuombea upate fanaka!

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania