Zaburi 131

Zaburi 131

Kumtumainia Mungu kwa utulivu

1Ee Mwenyezi-Mungu, sina moyo wa kiburi;

mimi si mtu wa majivuno.

Sijishughulishi na mambo makuu,

au yaliyo ya ajabu mno kwangu.

2Ila nafsi yangu imetulia na kuwa na amani,

kama mtoto mchanga alivyotulia na mama yake;

ndivyo nafsi yangu ilivyo tulivu.

3Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,

tangu sasa na hata milele.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania