Zaburi 101

Zaburi 101

Zaburi 101

Ahadi ya kuishi kwa uadilifu na kwa haki

1Nitaimba kuhusu upendo wako na haki yako;

kwako wewe, Ee Mwenyezi Mungu, nitaimba sifa.

2Nitazingatia kuishi maisha yasiyo na lawama:

utakuja kwangu lini?

Nitatembea nyumbani mwangu

kwa moyo usio na lawama.

3Sitaweka mbele ya macho yangu

kitu kiovu.

Ninayachukia matendo ya watu wasio na imani;

hawatashikamana nami.

4Moyo wa ukaidi utakuwa mbali nami;

nitajitenga na kila ubaya.

5Kila amsingiziaye jirani yake kwa siri,

huyo nitamnyamazisha;

mwenye macho ya dharau na moyo wa kiburi

huyo sitamvumilia.

6Macho yangu yatawaelekea waaminifu katika nchi,

ili waweze kuishi pamoja nami;

yeye ambaye moyo wake hauna lawama

atanitumikia.

7Mdanganyifu hatakaa

nyumbani mwangu,

yeye asemaye kwa uongo

hatasimama mbele yangu.

8Kila asubuhi nitawanyamazisha

waovu wote katika nchi;

nitamkatilia mbali kila mtenda maovu

kutoka mji wa Mwenyezi Mungu.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.