Zaburi 121

Zaburi 121

Zaburi 121

Mwenyezi Mungu mlinzi wetu

1Nayainua macho yangu natazama milima:

msaada wangu utatoka wapi?

2Msaada wangu hutoka kwa Mwenyezi Mungu,

Muumba wa mbingu na dunia.

3Hatauacha mguu wako uteleze,

yeye akulindaye hatasinzia,

4hakika, yeye alindaye Israeli

hatasinzia wala hatalala usingizi.

5Mwenyezi Mungu anakulinda,

Mwenyezi Mungu ni uvuli wako mkono wako wa kuume,

6jua halitakudhuru mchana,

wala mwezi wakati wa usiku.

7Mwenyezi Mungu atakukinga na madhara yote,

atayalinda maisha yako,

8Mwenyezi Mungu atakulinda unapoingia na unapotoka,

tangu sasa na hata milele.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.