Zaburi 129

Zaburi 129

Zaburi 129

Maombi dhidi ya adui za Israeli

1Wamenitesa sana tangu ujana wangu;

Israeli na aseme sasa:

2wamenitesa sana tangu ujana wangu,

lakini bado hawajanishinda.

3Wakulima wamelima mgongo wangu,

na kufanya mifereji yao mirefu.

4Lakini Mwenyezi Mungu ni mwenye haki;

amenifungua toka kamba za waovu.

5Wale wote wanaoichukia Sayuni

na warudishwe nyuma kwa aibu.

6Wawe kama majani juu ya paa,

ambayo hunyauka kabla hayajakua;

7kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake,

wala akusanyaye kujaza mikono yake.

8Wale wapitao karibu na wasiseme,

“Baraka ya Mwenyezi Mungu iwe juu yako;

tunakubariki katika jina la Mwenyezi Mungu.”

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.