Zaburi 130

Zaburi 130

Zaburi 130

Kumngojea Mwenyezi Mungu

1Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Mwenyezi Mungu.

2Ee Bwana, sikia sauti yangu.

Masikio yako na yawe masikivu

kwa kilio changu unihurumie.

3Kama wewe, Ee Mwenyezi Mungu, ungeweka kumbukumbu ya dhambi,

Ee Bwana, ni nani angeweza kusimama?

4Lakini kwako kuna msamaha,

kwa hiyo wewe unaogopwa.

5Namngojea Mwenyezi Mungu, nafsi yangu inangojea,

katika neno lake naweka tumaini langu.

6Nafsi yangu inamngojea Bwana

kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi,

naam, kuliko walinzi

waingojeavyo asubuhi.

7Ee Israeli, mtumaini Mwenyezi Mungu,

maana kwa Mwenyezi Mungu kuna upendo usiokoma,

na kwake kuna ukombozi kamili.

8Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli

kutoka dhambi zao zote.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.