Zaburi 6

Zaburi 6

Zaburi 6

Sala ya kuomba msaada wakati wa taabu

1Ee Bwana , usinikemee katika hasira yako,

wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.

2Unirehemu Bwana ,

kwa maana nimedhoofika;

Ee Bwana , uniponye,

kwa maana mifupa yangu

ina maumivu makali.

3Nafsi yangu ina uchungu mwingi.

Hadi lini, Ee Bwana , hadi lini?

4Geuka, Ee Bwana , unikomboe,

uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.

5Hakuna mtu anayekukumbuka

akiwa amekufa.

Ni nani awezaye kukusifu

akiwa Kuzimu?

6Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni;

usiku kucha natiririsha

kitanda changu kwa machozi;

nimelowesha kiti changu

kwa machozi yangu.

7Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika,

yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.

8Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya,

kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.

9Bwana amesikia kilio changu kwa huruma,

Bwana amekubali sala yangu.

10Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika,

watarudi nyuma na waaibishwe kwa ghafula.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.