Zaburi 13

Zaburi 13

Sala ya ukombozi kutoka kwa adui

1Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele?[#Kum 31:17; Ayu 13:24; Zab 22:1; Isa 59:2]

Hadi lini utanificha uso wako?

2Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini,

Nikihuzunika moyoni mchana kutwa?

Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini?

3Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie;[#Ezr 9:8; Zab 18:28; Lk 2:32; Ufu 21:23; Zab 76:5,6; Isa 37:36; Yer 51:39; Efe 5:14]

Uyatie nuru macho yangu,

Nisije nikalala usingizi wa mauti.

4Adui yangu asije akasema, Nimemshinda;

Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.

5Lakini mimi nimezitumainia fadhili zako;[#2 Nya 20:12]

Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.

6Naam, nitamwimbia BWANA,

Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.

The Holy Bible in Kiswahili, Revised Union Version © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 2013. 
Published by: Bible Society of Tanzania