The chat will start when you send the first message.
1Ee BWANA, uisikie sala yangu, uzisikilize dua zangu Unijibu Kwa uaminifu wako,
Unijibu kwa haki yako.
2Wala usimhukumu mtumishi wako,[#Ayu 14:3; 4:17; Mhu 7:20; Rum 3:20; Gal 2:16]
Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki.
3Maana adui ameifuatia nafsi yangu,[#Zab 7:1-2]
Ameutupa chini uzima wangu.
Amenikalisha mahali penye giza,
Kama watu waliokufa zamani.
4Na roho yangu imezimia ndani yangu,[#Zab 61:2]
Moyo wangu ndani yangu umeshtuka.
5Nimezikumbuka siku za kale,[#Zab 77:5,11]
Nimeyatafakari matendo yako yote,
Naziwaza kazi za mikono yako.
6Nakunyoshea mikono yangu;[#Zab 28:2]
Nafsi yangu inakuonea kiu kama nchi kame.
7Ee BWANA, unijibu hima, roho yangu imelegea;
Usinifiche uso wako,
Nisifanane nao washukao shimoni.
8Uniwezeshe kusikia fadhili zako asubuhi,
Kwa maana nimekutumaini Wewe.
Unifundishe njia nitakayoiendea,
Kwa maana ninakuinulia nafsi yangu.
9Ee BWANA, uniponye na adui zangu;
Nimekukimbilia Wewe, unifiche.
10Unifundishe kuyatenda mapenzi yako,[#Zab 25:4; Yn 14:26; Rum 5:5; Efe 4:30; Gal 5:22-23]
Kwa maana ndiwe Mungu wangu;
Roho yako mwema aniongoze katika njia iliyo sawa,
11Ee BWANA, uniponye kwa ajili ya jina lako,
Kwa haki yako unitoe roho yangu taabuni;
12Kwa fadhili zako utawakatilia mbali adui zangu;
Na kuwaangamiza wote wanitesao nafsi,
Kwa maana mimi ni mtumishi wako.