Zaburi 76

Zaburi 76

Mungu wa Waisraeli - Mungu mkuu

1Katika Yuda Mungu amejulikana,

Katika Israeli jina lake ni kuu.

2Kibanda chake pia kiko Salemu,

Na maskani yake iko Sayuni.

3Huko ndiko alikoivunja mishale ya uta,[#Zab 46:9; Eze 39:9]

Ngao, upanga, na zana za vita.

4Wewe U mwenye fahari na adhama,[#Eze 38:12]

Toka milima ya mateka.

5Wametekwa wenye moyo thabiti;[#Isa 46:12; Zab 13:3; Yer 51:39]

Wamelala usingizi;

Wala hawakuiona mikono yao

Watu wote walio hodari.

6Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo,[#Kut 15:1; Nah 2:13; Zek 12:4]

Gari na farasi wameshikwa na usingizi mzito.

7Wewe ndiwe utishaye, naam, Wewe;[#Ayu 41:10; Nah 1:6]

Naye ni nani awezaye kusimama ukasirikapo?

8Toka mbinguni ulitangaza hukumu;

Nchi iliogopa, ikakaa kimya.

9Mungu aliposimama ili kuhukumu

Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia.

10Maana hasira ya binadamu itakusifu,[#Kut 9:16]

Masalio ya hasira utajifunga kama mshipi.

11Wekeni nadhiri na mziondoe[#Mhu 5:4; Zab 68:29]

Kwa BWANA, Mungu wenu.

Wote wanaomzunguka wamletee hedaya,

Yeye astahiliye kuogopwa.

12Yeye huzikata roho za wakuu;[#Zab 68:35]

Na kuwatisha wafalme wa dunia.

The Holy Bible in Kiswahili, Revised Union Version © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 2013. 
Published by: Bible Society of Tanzania