Mashangilio 11

Mashangilio 11

Mungu ni mwongofu.

1Bwana ndiye, nimkimbiliaye, nanyi mnaiambiaje roho yangu: Rukia mlimani kama ndege?[#1 Sam. 26:20.]

2Kwani watazameni wasiomcha Mungu, wanapinda pindi, wakapachika mishale penye upote, wapige gizani wanyokao mioyo.[#Sh. 37:14; 64:4-5.]

3Misingi inapobomolewa, mwongofu atafanyaje?

4Bwana yumo Jumbani mwake mwenye utakatifu, yeye Bwana kiti chake cha uamuzi kiko mbinguni, macho yake huwachungulia wana wa watu, kope zake ziwajaribu.[#Sh. 33:13-14; Yes. 66:1; Hab. 2:20.]

5Bwana humjaribu naye mwongofu, roho yake humchukia asiyemcha naye apendaye ukorofi.[#Sh. 5:5.]

6Atawanyeshea matanzi wao wasiomcha, tena mvua za moto na za viberitiberiti, nao upepo wa kuchoma moto ndio kinywaji, watakachogawiwa.[#1 Mose 19:24.]

7Kwani Bwana ni mwongofu, hupenda yaongokayo; kwa hiyo anyokaye moyo atauona uso wake.[#Sh. 17:15; 33:5; Mat. 5:8.]

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania