The chat will start when you send the first message.
1Niamulie, Mungu, ukinigombea kondo yangu kwao wasionipenda! Niopoe mikononi mwao wenye uwongo namo mwao wapotovu![#Sh. 26:1.]
2Kwani wewe Mungu uliye nguvu yangu, mbona umenitupa? Mbona sina budi kwenda na kusikitika, adui anaponisonga?[#Sh. 42:10.]
3Tuma mwanga wako na kweli yako, ije kuniongoza na kunipeleka kwenye mlima wako mtakatifu, Kao lako liliko.[#Sh. 15:1.]
4Niingie mwenye meza ya kumtambikia Mungu wangu, ni yule Mungu, ninayemfurahia na kumpigia vigelegele. Nitakushukuru na kukupigia zeze, Mungu uliye Mungu wangu.[#Sh. 63:6.]
5Mbona unajihangaisha, roho yangu, ukivuma ndani yangu? Mngoje Mungu na kumtazamia, kwani siku itakuja, nitakapomshukuru kwa kuokolewa nao uso wake.[#Sh. 42:5,11.]