Zaburi 122

Zaburi 122

Wimbo wa sifa na sala kwa Yerusalemu

1Nilifurahi waliponiambia,[#Isa 2:3; Yer 31:6; Zek 8:21]

Twende nyumbani kwa BWANA.

2Miguu yetu imesimama

Ndani ya malango yako, Ee Yerusalemu.

3Ee Yerusalemu uliyejengwa[#2 Sam 5:9; Efe 2:21]

Kama mji ulioshikamana,

4Huko ndiko wapandako kabila,[#Kum 16:16; Kut 16:34]

makabila ya BWANA;

Kama ulivyowaamuru Waisraeli,

Walishukuru jina la BWANA.

5Maana huko viliwekwa viti vya hukumu,

Viti vya enzi vya ukoo wa Daudi.

6Uombeeni Yerusalemu amani;[#Isa 62:6; Yer 51:50]

Na wafanikiwe wakupendao;

7Amani na ikae ndani ya kuta zako,

Na kufanikiwa ndani ya majumba yako.

8Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu

Niseme sasa, Amani ikae nawe.

9Kwa ajili ya nyumba ya BWANA, Mungu wetu,

Nitakuombea mema.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya