Zab 137

Zab 137

Maombolezo juu ya Maangamizi ya Yerusalemu

1Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,[#Eze 1:1; Dan 8:2; Isa 24:8; Omb 5:15; Amo 8:10; Ufu 18:22]

Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.

2Katika miti iliyo katikati yake

Tulivitundika vinubi vyetu.

3Maana huko waliotuchukua mateka

Walitaka tuwaimbie;

Na waliotuonea walitaka furaha;

Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.

4Tuuimbeje wimbo wa BWANA

Katika nchi ya ugeni?

5Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe,

Mkono wangu wa kuume na usahau.

6Ulimi wangu na ugandamane[#Eze 3:26]

Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.

Nisipoikuza Yerusalemu

Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.

7Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,[#Omb 4:22; Oba 1:10]

Siku ya Yerusalemu.

Waliosema, Bomoeni!

Bomoeni hata misingini!

8Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,[#Isa 13:1; Ufu 18:6]

Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.

9Heri yeye atakayewakamata wadogo wako,

Na kuwaseta wao juu ya mwamba.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania