The chat will start when you send the first message.
1Kando ya mito ya Babeli ndiko tulikoketi,[#Eze 1:1; Dan 8:2; Isa 24:8; Omb 5:15; Amo 8:10; Ufu 18:22]
Tukalia tulipoikumbuka Sayuni.
2Katika miti iliyo katikati yake
Tulivitundika vinubi vyetu.
3Maana huko waliotuchukua mateka
Walitaka tuwaimbie;
Na waliotuonea walitaka furaha;
Tuimbieni baadhi ya nyimbo za Sayuni.
4Tuuimbeje wimbo wa BWANA
Katika nchi ya ugeni?
5Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe,
Mkono wangu wa kuume na usahau.
6Ulimi wangu na ugandamane[#Eze 3:26]
Na kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.
Nisipoikuza Yerusalemu
Zaidi ya furaha yangu iliyo kuu.
7Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,[#Omb 4:22; Oba 1:10]
Siku ya Yerusalemu.
Waliosema, Bomoeni!
Bomoeni hata misingini!
8Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,[#Isa 13:1; Ufu 18:6]
Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.
9Heri yeye atakayewakamata wadogo wako,
Na kuwaseta wao juu ya mwamba.