Zab 47

Zab 47

Utawala wa Mungu juu ya Mataifa

1Enyi watu wote, pigeni makofi,

Mpigieni Mungu kelele kwa Sauti ya shangwe.

2Kwa kuwa BWANA Aliye juu, mwenye kuogofya,[#Kum 7:21; Neh 1:5; Mal 1:14]

Ndiye mfalme mkuu juu ya dunia yote.

3Atawatiisha watu wa nchi chini yetu,[#Zab 18:47]

Na mataifa chini ya miguu yetu.

4Atatuchagulia urithi wetu,[#1 Pet 1:4]

Fahari ya Yakobo ambaye alimpenda.

5Mungu amepaa kwa kelele za shangwe,[#Zab 24:7-10; Mdo 1:9; Efe 4:8-10; 1 Tim 3:16]

BWANA kwa sauti ya baragumu.

6Mwimbieni Mungu, naam, imbeni;

Mwimbieni mfalme wetu, naam, imbeni.

7Maana Mungu ndiye mfalme wa dunia yote,[#Zek 14:9; 1 Kor 14:15]

Imbeni kwa akili.

8Mungu awamiliki mataifa,

Mungu ameketi katika kiti chake kitakatifu.

9Wakuu wa watu wamekusanyika,

Wawe watu wa Mungu wa Ibrahimu.

Maana ngao za dunia zina Mungu,

Ametukuka sana.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania