Zaburi 13

Zaburi 13

Kuomba msaada

1Mpaka lini ee Mwenyezi-Mungu, utanisahau?

Je, utanisahau mpaka milele?

Mpaka lini utanificha uso wako?

2Nitakuwa na wasiwasi rohoni hadi lini,

na sikitiko moyoni siku hata siku?

Hadi lini adui zangu watafurahia taabu zangu?

3Uniangalie na kunijibu, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu.

Uyaangazie macho yangu, nisipatwe na usingizi wa kifo.

4Usiwaache maadui zangu waseme: “Tumemweza huyu!”

Watesi wangu wasije wakafurahia kuanguka kwangu.

5Lakini mimi nazitumainia fadhili zako;

moyo wangu na ufurahie wokovu wako.

6Nitakuimbia wewe, ee Mwenyezi-Mungu,

kwa ukarimu mwingi ulionitendea!

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania