Zaburi 130

Zaburi 130

Kuomba msaada

1Toka upeo wa unyonge wangu,

nakulilia, ee Mwenyezi-Mungu.

2Ee Bwana, sikia sauti yangu,

uitegee sikio sauti ya ombi langu.

3Kama, ee Mwenyezi-Mungu ungekumbuka maovu yetu

nani, ee Bwana, angeweza kusalimika?

4Lakini kwako twapata msamaha,

ili sisi tukuheshimu.

5Namtumainia Mwenyezi-Mungu kwa moyo wangu wote;

nina imani sana na neno lake.

6Ninamtumainia Mwenyezi-Mungu

kuliko walinzi wanavyongojea pambazuko;

kuliko walinzi wanavyongojea kuche asubuhi.

7Ee Israeli, umtumainie Mwenyezi-Mungu,

maana kwake Mwenyezi-Mungu kuna fadhili,

kwake kuna nguvu kubwa ya kutukomboa.

8Yeye atawakomboa watu wa Israeli[#Taz Mat 1:21; Tito 2:14]

kutoka katika maovu yao yote.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania