Zaburi 23

Zaburi 23

Mungu mchungaji wangu

1Mwenyezi-Mungu ni mchungaji wangu,

sitapungukiwa na kitu.

2Hunipumzisha kwenye malisho mabichi;

huniongoza kando ya maji matulivu,

3na kuirudishia nafsi yangu nguvu mpya.

Huniongoza katika njia sawa

kwa hisani yake.

4Nijapopita katika bonde la giza kuu la kifo,

sitaogopa hatari yoyote,

maana wewe ee Mwenyezi-Mungu u pamoja nami;

gongo lako na fimbo yako vyanilinda.

5Umeniandalia karamu mbele ya maadui zangu;

umenipaka mafuta kichwani pangu;

kikombe changu umekijaza mpaka kufurika.

6Kweli wema wako na fadhili zako zitakuwa pamoja nami,

siku zote za maisha yangu;

nami nitakaa nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu milele.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania