Zaburi 82

Zaburi 82

Mungu mtawala mkuu

1Mungu anasimamia baraza lake;

anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu:

2“Mpaka lini mtaendelea kuhukumu bila haki

na kuwapendelea watu waovu?

3Wapeni wanyonge na yatima haki zao;

tekelezeni haki za wanaoonewa na fukara.

4Waokoeni wanyonge na maskini,

waokoeni makuchani mwa wadhalimu.

5“Lakini nyinyi hamjui wala hamfahamu!

Nyinyi mnatembea katika giza la upotovu!

Misingi yote ya haki duniani imetikiswa!

6Mimi nilisema kuwa nyinyi ni miungu;

kwamba nyote ni watoto wa Mungu Mkuu!

7Hata hivyo, mtakufa kama watu wote;

mtaanguka kama mkuu yeyote.”

8Inuka ee Mungu, uuhukumu ulimwengu;

maana mataifa yote ni mali yako.

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki -1995, 2001: kwa Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania