Zaburi 110

Zaburi 110

Kutawazwa kwa mfalme mteule

1Mwenyezi-Mungu amwambia bwana wangu:

“Keti upande wangu wa kulia,

hata niwaweke maadui zako chini ya miguu yako.”

2Mwenyezi-Mungu ataeneza enzi yako kutoka Siyoni;

utatawala juu ya maadui zako wote.

3Watu wako watakujia kwa hiari,

siku utakapokwenda kuwapiga maadui.

Juu ya milima mitakatifu watakujia vijana wako,

kama umande unaotokeza alfajiri mapema.

4Mwenyezi-Mungu amekuapia wala hatabadili nia yake:

“Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”

5Bwana yuko upande wako wa kulia;

atawaponda wafalme atakapokasirika.

6Atayahukumu mataifa na kuwaua watu wengi;

atawaponda viongozi kila mahali duniani.

7Mfalme atakunywa maji ya kijito njiani;[#110:7 Maana ya maneno haya si dhahiri. Wengine wanafikiri ataweza kunywa maji popote maana atakuwa amepata ushindi kila mahali.]

naye atainua kichwa juu kwa ushindi.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania