Zaburi 123

Zaburi 123

Kuomba huruma

1Nakutazamia kwa hamu, ee Mwenyezi-Mungu,

nakuangalia wewe utawalaye huko juu mbinguni!

2Kama watumishi wamtegemeavyo bwana wao,

kama mjakazi amtegemeavyo bibi yake,

ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe,

ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu,

mpaka hapo utakapotuonea huruma.

3Utuhurumie, ee Mwenyezi-Mungu, utuhurumie,

maana tumedharauliwa kupita kiasi.

4Tumeshiba muda mrefu dharau za matajiri,

tumepuuzwa mno na wenye kiburi.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania