Zaburi 134

Zaburi 134

Msifuni Mungu

1Njoni kumsifu Mwenyezi-Mungu enyi watumishi wake wote,

enyi nyote mnaotumikia usiku nyumbani mwake.

2Inueni mikono kuelekea mahali patakatifu,

na kumtukuza Mwenyezi-Mungu!

3Mwenyezi-Mungu awabariki kutoka Siyoni;[#134:3 Maneno haya huenda yalitamkwa na kuhani kuwatakia baraka mahujaji waliofika Yerusalemu kwa sikukuu fulani. Taz pia 104.]

yeye aliyeumba mbingu na dunia.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania