The chat will start when you send the first message.
1Wapumbavu hujisemea moyoni:[#14:1 Neno la Kiebrania lililotafsiriwa hapa kama “mpumbavu” katika mazingira haya linamtaja mtu ambaye kimsingi ni mwovu. Mpumbavu hamtegemei Mungu na hana upendo kwa watu, na hana hekima (Mhub 2:14).]
“Hakuna Mungu.”
Wote wamepotoka kabisa,
wametenda mambo ya kuchukiza;
hakuna hata mmoja atendaye jema!
2Mwenyezi-Mungu anawaangalia wanadamu kutoka mbinguni,
aone kama kuna yeyote mwenye busara,
kama kuna yeyote anayemtafuta Mungu.
3Lakini wote wamekosa,
wote wamepotoka pamoja;
hakuna atendaye mema,
hakuna hata mmoja.
4“Je, hao watendao maovu hawana akili?
Wanawatafuna watu wangu kama mikate;
wala hawanijali mimi Mwenyezi-Mungu.”
5Hapo watashikwa na hofu kubwa,
maana Mungu yu pamoja na waadilifu.
6Unaweza kuvuruga mipango ya maskini,[#14:6 Taz 9:8-9 na 12:5 maelezo.]
lakini Mwenyezi-Mungu ndiye kimbilio lake.
7Laiti ukombozi wa Israeli ungefika kutoka Siyoni!
Mwenyezi-Mungu atakaporekebisha hali ya watu wake,
wazawa wa Yakobo watashangilia;
Waisraeli watafurahi.