Zaburi 124

Zaburi 124

Zaburi 124

Shukrani kwa ukombozi wa Israeli

1Kama Mwenyezi Mungu hangekuwa upande wetu;

Israeli na aseme sasa:

2kama Mwenyezi Mungu hangekuwa upande wetu,

watu walipotushambulia,

3hasira yao ilipowaka dhidi yetu,

wangetumeza tukiwa hai,

4mafuriko yangegharikisha,

maji mengi yangetufunika,

5maji yaendayo kasi

yangetuchukua.

6Ahimidiwe Mwenyezi Mungu,

ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.

7Tumeponyoka kama ndege

kutoka mtego wa mwindaji;

mtego umevunjika,

nasi tumeokoka.

8Msaada wetu ni katika jina la Mwenyezi Mungu,

Muumba wa mbingu na dunia.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.