Zaburi 134

Zaburi 134

Zaburi 134

Wito wa kumsifu Mwenyezi Mungu

1Msifuni Mwenyezi Mungu, ninyi nyote watumishi wa Mwenyezi Mungu,

ninyi mnaotumika usiku ndani ya nyumba ya Mwenyezi Mungu.

2Inueni mikono yenu katika patakatifu

na kumsifu Mwenyezi Mungu.

3Naye Mwenyezi Mungu, Muumba wa mbingu na dunia,

awabariki kutoka Sayuni.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.