Zaburi 63

Zaburi 63

Zaburi 63

Shauku kwa ajili ya uwepo wa Mungu

1Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu,

nakutafuta kwa moyo wote;

nafsi yangu inakuonea kiu,

mwili wangu unakuonea wewe shauku,

katika nchi kame na iliyochoka,

mahali pasipo maji.

2Nimekuona katika mahali patakatifu

na kuuona uwezo wako na utukufu wako.

3Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai,

midomo yangu itakuadhimisha.

4Nitakusifu siku zote za maisha yangu,

na kwa jina lako nitainua mikono yangu.

5Nafsi yangu itatoshelezwa,

kama kushiba vyakula vizuri;

kwa midomo iimbayo

kinywa changu kitakusifu wewe.

6Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe;

ninakuwaza makesha yote ya usiku.

7Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu,

chini ya uvuli wa mabawa yako naimba.

8Nafsi yangu inaambatana nawe,

mkono wako wa kuume hunishika.

9Wale wanaotafuta uhai wangu wataangamizwa;

wataenda chini kwenye vilindi vya dunia.

10Watatolewa wafe kwa upanga,

nao watakuwa chakula cha mbweha.

11Bali mfalme atafurahi katika Mungu,

wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu,

bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.

Neno: Biblia Takatifu™ Neno™ Hakimiliki © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Version™ Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015, 2025 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.